Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu kwa mnasaba wa siku ya saba tangu kuuawa shahidi makumi ya wananchi wa Zahedan
Taasisi zote husika zinapaswa kuwapa wafitini jaza yao kwa uhalifu waliotenda
2010/07/21 - 17:14
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei leo ametoa ujumbe kwa mnasaba wa kutimia siku ya saba tangu kuuawa shahidi makumi ya wananchi waumini wa mji wa Zahedan huko kusini mashariki mwa Iran katika milipuko ya kigaidi iliyolenga msikiti mkuu wa mji huo akivitaja vyombo vya ujasusi vya Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Uingereza kuwa ndio wahusika wakuu wa jinai hiyo. Ayatullah Khamenei amesema kuwa moja ya malengo makuu ya maadui katika kutekeleza shambulio hilo la kigaidi ni kuzusha hitilafu na fitina za kimadhehebu lakini Jamhuri ya Kiislamu haitaruhusu mikono ya ubeberu wa kimataifa kufikia lengo lake. Vilevile amevitaka vyombo vyote husika vya Serikali, Bunge na Mahakama kupambana vilivyo na maadui wa umoja na usalama wa taifa na kuwafikisha wahalifu mbele ya sheria.